Thank you for taking your time to find out more about the blog. This blog is your number one event, sports, advertisement and entertainment news. Welcome to an Entertainment revolution. Advertisement gate way and promotion as well, STAY ON IT ENJOY CALL / SMS +255 686 123425 for more information and any blog assistance
Wednesday, 7 November 2012
BARCELONA NDIYO CLUB BORA DUNIANI IKIFUATIWA NA ATLETICO MADRID , ESPERANCE NDIO BORA AFRICA
SHIRIKISHO la Kimataifa la Soka la Historia na Takwimu-IFFHS ambalo linahusika na utunzaji wa historia na kumbukumbu za soka limetoa orodha ya mwezi Octoba mwaka huu ya vilabu 400 bora duniani. Katika orodha hizo klabu ya Barcelona bado imeendelea kukaa kileleni ikiwa na alama 349 ikifuatiwa na klabu ya Atletico Madrid wakishika nafasi ya pili wakiwa na alama 290 huku ya tatu ikiwa klabu ya CD Universidad de Chile Santiago ambayo imedondoka nafasi moja kutoka nafasi ya pili waliyokuwepo msimu Septemba mpaka nafasi ya tatu. Klabu nyingine ni Boca Juniors ya Argentina ambayo nayo imeshuka kwa nafasi moja kutoka ya tatu waliyokuwepo Septemba wakiwa na alama 276 na tano bora inafungwa na Real Madrid ambayo imejikusanyia alama 271. Kwa upande wa Afrika klabu ya Esperance ya Tunisia bado imeendelea kuongoza wakiwa nafasi ya 61 wakifuatiwa na Al Hilal Omdurman ya Sudan ambao wako nafasi ya 82 huku klabu nyingine ya Sudan Al-Merreikh Omdurman ikifuatia katika nafasi ya tatu kwa upande wa Afrika na 117 duniani. Chelsea Berekum ya Ghana inashika nafasi ya nne kwa upande wa Afrika huku duniani nayo pia ikishika nafasi ya 117 na tano bora inafungwa na Wydad Casablanca ya Morocco ambayo iko katika nafasi ya 141 duniani.

Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment