Wanafunzi wapatao 344 wa shule ya sekondari ya wasichana Masasi mkoani
Mtwara wameandamana hadi nyumbani kwa Mkuu wa wilaya ya Masasi, Farida
Mgomi wakishinikiza kuondolewa kwa mkuu wa shule hiyo, Reinader Tesha
kufuatia kifo cha mwanafunzi mwenzao wa kidato cha tano Omega Kabuje
aliyefariki jana (Jumamosi), FikraPevu imeelezwa.
Wakati wanafunzi hao wakiwa katika maandamano ambayo yaliyofanyika
leo(jumapili) kuanzia saa 11 alfajiri ambayo hata hivyo hawakufanikiwa
kukutana na mkuu wa wilaya, Mgomi kwani alikuwa safarini Mtwara, mkuu
wa shule hiyo ya wasichana Reinader Tesha alijikuta akipoteza fahamu na
kukimbizwa hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Masasi ya Mkomaindo
ambapo anaendelea kupata matibabu baada ya kuanguka ghafla akiwa
nyumbani kwake baada ya kujifungia kwa takribani saa nne.
Hatua ya wanafunzi hao ambayo imekuja wakati tume iliyoundwa na baraza
la madiwani kuchunguza malalamiko yanayomhusu mkuu wa shule hiyo jinsi
anavyowanyanyasa wananfunzi wake na utendaji wake wa kazi hasa tuhuma za
manyanyaso yanyofanyiwa wanafunzi wa shule hiyo.
Akizungumza kwa niaba ya wanafunzi wenzake, Dada mkuu wa shule hiyo,
Regina Christopher alibainisha kuwa wamechukua hatua hiyo baada ya
kuchoshwa na vitendo vya mkuu huyo ambapo mara zote amekuwa
anawanyanyasa na kutowathamini pindi wanapokuwa wagonjwa na walimu wa
kutowajali wanafunzi.
Alidai kuwa mkuu huyo wa shule amekuwa hafuatilii wanapougua ambapo
jukumu linakuwa la wanafunzi wenyewe kutafuta usafiri wa kuwapeleka
hospitali kwa ajili ya kupata matibabu kwani shule haijishughulishi na
huduma za matibabu.
“Mwenzetu amefariki leo na hii tunajua si kwa mipango ya Mungu bali
kuna uzembe wa walimu na watoa huduma hivyo tumeamua leo kuandamana hadi
kwa Mkuu wa Wilaya kuonesha kukerwa na tabia hizo,” alisema Regina.
Kiongozi huyo wa shule pia alilalalamikia huduma mbovu inatolewana
wahudumu wa hospitali ya wilaya wananfunzi hao wanapofika kupata huduma
za matibabu ambapo wahudumu hao huwa wanawatolea maneno ya dharau na
kejeli hali ambayo pia inaweza kuwa ilichangia kifo cha mwanafunzi
mwenzao.
Akizungumzia tukio hilo Makamu mkuu wa shule hiyo, Vestina Nditi
alikiri kutokea mgogoro huo na kuwa ulitokana baada ya mwanafunzi wa
kidato cha tano Omega Kabuje kufariki akiwa hospitali.
Hata hivyo, alisema ya kuwa malalamikio yaliyotolewa na wanafunzi si ya
kweli kwani uongozi wa shule unajitahidi kuwapatia huduma mbalimbali
wanapokuwa wagonjwa na kuwa tatizo kwa sasa shule hiyo haina mlezi
ambaye ana taaluma ya uuguzi.
“Hizo taarifa si sahihi kwani kwa uwezo wetu walimu tunajitahidi
kuwahudumia wanafunzi ila tatizo shule kwa sasa haina mlezi mwenye
taaluma ya uuguzi ingawa tumeahidiwa na halmashauri kuwa tutampata hivi
karibuni,” alisema Nditi.
Kwa upande wake Mganga mkuu wa hospitali ya halmashauri ya mji wa
Masasi, Dkt Harry Mwambe alikiri hospitali yake kumpokea mwanafunzi huyo
siku ya ijumaa saa kumi na moja jioni ambapo baada ya uchunguzi wa
vipimo vya kitabibu alibainika kuwa alikuwa na malaria kali na jana
(Jumamosi) saa 10.15 alifariki dunia.
Akizungumzia malalamiko yaliyotolewa na wananfunzi hao, Mganga mkuu
huyo alisema kuwa hana taarifa juu ya malalamiko hayo na kuwa
atayashulikia na kama ikibainika yana ukweli atachukua hatua kali kwa
wale wenye tabia hizo
Thank you for taking your time to find out more about the blog. This blog is your number one event, sports, advertisement and entertainment news. Welcome to an Entertainment revolution. Advertisement gate way and promotion as well, STAY ON IT ENJOY CALL / SMS +255 686 123425 for more information and any blog assistance
Monday, 12 May 2014
WANAFUNZI WA MASASI GIRLS - MTWARA WAANDAMANA KUPINGA KIFO CHA MWANAFUNZI MWENZAO KILICHOSABABISHWA NA UZEMBE WA MWALIMU MKUU
An Entertainer and the Owner of 60Entertainment who is near by to present TV program on local TV, Current am working with One of the Biggest company
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment