viongozi
wa klabu ya Young Africans unapenda kuwajulisha wanachama wake, wapenzi
wa soka na wadau kwa ujumla kuwa taarifa za kuhama kwa wachezai wake
Didier Kavumbagu na Frank Domayo kwenda kujiunga na Azam FC
zisiwakatishe tamaa, ni mapenzi ya wachezaj wenyewe kwani
walishakubaliana na uongozi kila kitu juu ya kuendelea kuitumikia Yanga
kabla ya siku mbili hizi kuonekana wakiwa wamejiunga na wana ramba
ramba.
Yanga tayari ina wachezaji watatu wenye mikataba inayoendelea na kama
kanuni za VPL kwa wachezai wa kimataifa kuwa watatu zitatumika
wachezaji Haruna Niyonzima, Hamisi Kizza na Emmanuel Okwi ndio
watakaoendelea, hivyo uongozi uliomba mwongozo kwa TFF juu ya taratibu
zitakazotumika kwa msimu ujao kabla ya kuwasainisha Kavumbagu na Twite.
Awali uongozi wa Yanga ulikuwa kwenye mazungumzo na wachezaji hao
tangu mwanzoni mwa msimu wa 2013/2014 juu ya kuongezewa muda wa mikataba
yao ili waweze kuendelea kuitumika Yanga kwa ajili msimu mpya ujao
2014/2015.
Didier Kavumbagu na Mbuyu Twite ambao mikataba yao ilikuwa mwishoni
waliongea na uongozi tangu mapema mwaka jana mwezi wa Septemba juu ya
kuweka sahihi zao na kuendelea kuitumikia Yanga na kukubaliana mambo
yote ya msingi kikubwa kilichokuwa kinasubiriwa ni maamuzi ya TFF juu ya
usajili wa wachezaji wa kigeni msimu mpya wa 2014/2015 kwani Azimio la
Bagamoyo linapaswa kuanza kutekelezwa msimu huu.
Uongozi wa Yanga uliandikia TFF barua mapema kuomba kupewa mwongozo
wa kanuni zitakazotumika kwenye usajli kwa wachezaji wa kimataifa kwa
msimu mpya kufuatia Azimio la Bagamoyo kuelekeza msimu huu kila timu
inapasa kuwa na wachezaji watatu wa kigeni, mpaka sasa uongozi wa Yanga
haujapata majibu juu ya utaratibu utakaotumika kwenye msimu wa Ligi Kuu
ijayo.
Hivyo makubaliano ya wachezaji Didier Kavumbagu, Mbuyu Twite na
uongozi wa Yanga SC yalikua yakisubira majibu ya TFF juu ya kanuni zipi
zitakazotumika kwenye usajili msimu wa 2014/2015 kwa wachezaji wa kigeni
na katika hali ya kushangaza Kavumbagu akaonekana tayari ameshasaini
kuichezea timu ya Azam FC.
Kuhusu Frank Domayo aliyeripotiwa jana kujiunga na Azam FC pia
alikuwa katika makubaliano ya kuongeza mkataa tangu mwezi Julai 2013,
alikubaliana na uongozi juu ya mambo yote ya msingi na kilichobakia
ilikuwa ni kuweka sahihi kwenye mkataba mpya, lakini Domayo alisema
hawezi kusaini mpaka siku atakapokuja mjomba wake ambaye ndie wakala
wake na ahadi hiyo iliendelea kwa muda wa mwaka mzima kabla ya jana
kusikia ameshasaini timu nyngine.
Habari hizi zimewashitua
wapenzi, wanachama na washabiki wa Young Africans lakini ukweli ni kuwa
wachezaji wenyewe walisindwa kuwa wakweli kwa viongozi na mwisho wa siku
walikua na mipango yao ya kuondoka, hivyo uongozi ulijtahid kadri ya
uwezo wake lakini wachezaji wanaonekana hawakua tayari kuendelea
kuichezea Yanga SC.
Taarifa kamili kuhusu mipango ya timu kwa
msimu ujao pamoja na ripoti ya kocha mkuu Hans pamoja na benchi lake la
Ufundi zitatolewa hivi karibuni baada ya benchi la ufundi na uongozi
kukaa kwa pamoja na kuafikiana mipango ya msimu ujao.
Aidha
uongozi wa Yanga SC unawaomba wanachama wake, wapenzi na washabiki
wasiwe na wasi wasi juu ya kuondoka kwa wachezaji hao kwani Yanga bado
ina nafasi wachezaji wengi wenye vipaji na itaendelea kuboresha kikosi
chake kwa kuzingatia maelekezo ya kocha mkuu Hans katika usajli wa msimu
ujao
Thank you for taking your time to find out more about the blog. This blog is your number one event, sports, advertisement and entertainment news. Welcome to an Entertainment revolution. Advertisement gate way and promotion as well, STAY ON IT ENJOY CALL / SMS +255 686 123425 for more information and any blog assistance
Friday, 2 May 2014
TAARIFA KAMILI KUHUSU USAJILI WA KAVUMBANGU na DOMAYO
An Entertainer and the Owner of 60Entertainment who is near by to present TV program on local TV, Current am working with One of the Biggest company
Subscribe to:
Post Comments (Atom)

No comments:
Post a Comment