Tuesday, 26 March 2013

KAJALA'S OUT

Habari ya taoo kwa sasa ni kumhusu bidada wa kuitwa Kajala ambaye leo amefanikiwa kunasuka katika ile kesi ambayo ilikuwa imemchukulia uhuru wake ambapo Leo hii amehukumiwa kwenda jela miaka mitano ama kulipa faini ya shilingi milioni 13 wakati Mumewe, Faraja Chambo akipata hukumu kubwa zaidi ya kwenda jela miaka 7 ama kulipa faini ya shilingi milioni 200 Relief na Habari nzuri kwa Kajala ilikuja pale wasanii wa Bongo Movie wapoonyesha kuwa tayari kuchanga hizo pesa za faini kwaajili ya kumtoa mwenzao, There then ikatokea Story nyingine tamu zaidi baada ya Bi dada Wema Sepetu kutokea mstari wa mbele na kuamua kulipa mpunga woote huo wa faini mwenyewe, kitu ambacho kimetafsiriwa kuwa ni upendo na ujasiri mkubwa na kumfanya .Kwa upande mwingine watu wameanza kujiuliza where is Wema getting all that 'Mulla' lakini kwa sasa kilichofanyika tayari kimefanyika (whats done is done) na Kajala anapumulia uraiani.

Kajala pamoja na muwewe faraja Chambo walikuwa wanakabiliwa na amakosa matatu ikiwepo kula njama na kuhamisha umiliki wa nyumba iliyopo Kunduchi Salasala isivyo halali na kutakatisha fedha haramu.



No comments: